Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani Tanzania

Mafunzo ya Ukufunzi kwa Wakufunzi

Imewekwa: 23 Dec, 2022
Mafunzo ya Ukufunzi kwa Wakufunzi

Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani Tanzania  Novemba 28, 2022 kilifunga rasmi  Mafunzo ya Ukufunzi kwa baadhi ya  Wakufunzi wa Kituo hicho. Washiriki wa Mafunzo hayo ni Maafisa na Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananch wa Tanzania(JWTZ) wanaofundisha kituoni hapo. Mafunzo hayo yalifungunguliwa Novemba 14, 2022 na yaliendeshwa kwa muda wa wiki mbili.



Aidha mafunzo hayo yaliandaliwa na JWTZ kwa ushirikiano na  Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Mafunzo na Utafiti (United Nations Institute of Training and Research - UNITAR) Akizungumza wakati wa kufunga Mafunxo hayo, Kaimu Mkuu wa Kituo hicho Kanali Deogratias Mulishi aliwashukuru UNITAR kwa kuwezesha Mafunzo hayo kwa Maafisa na Askari wa Jeshi hilo 

ReplyForward